Wednesday, October 31, 2012

JK USO KWA USO JIMBONI KWA MBOWE

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mbunge wa Hai ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe wakati rais alipowasili wilayani Hai kwa ajili ya kuzindua ujenzi wa barabara ya Hai-Masama mkoani Kilimanjaro.

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Hai, Novatus Makunga wakati alipowasili wilayani humo kwa ajili ya uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Hai_Masama mkoani Kilimanjaro.

Tuesday, October 30, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

1.  Kamati ya Ligi jana (Oktoba 29,2012) ilifanya kikao pamoja na klabu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom kujadili mambo kadhaa, likiwemo tukio la Jumamosi iliyopita la kuzuia televisheni na radio kutangaza moja kwa moja michezo ya Ligi Kuu pamoja na wapiga picha za televisheni kuchukua picha kwa ajili ya kutumia kwenye habari. Kamati ilifanya mazungumzo na mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA), Juma Pinto kuhusu msukosuko huo na kufikia muafaka katika masuala yafuatayo:
a-    kwamba uamuzi wa kuzuia vituo vya redio na televisheni kutangaza moja kwa moja ulikuwa sahihi lakini una kasoro katika utekelezaji kwa kuwa hayakuwepo mawasiliano rasmi kwa vyombo vya habari na pia haukutoa muda wa kutosha kwa vyombo hivyo vya habari kufanya maandalizi kwa kadri ya utashi wa klabu za Ligi Kuu.

b-    Kwamba Kamati ya Ligi haijakataza redio kutangaza moja kwa moja michezo ya Ligi Kuu, bali vituo vya redio ambavyo vinataka kutangaza moja kwa moja michezo ya Ligi Kuu vifanye hivyo bila ya kuweka matangazo ya wadhamini na kama matangazo hayo ya moja kwa moja yatadhaminiwa, basi vituo hivyo havina budi kuwasiliana kwa maandishi na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa maelekezo zaidi.

c-    Kwamba vituo vya redio vitakavyotaka kutangaza moja kwa moja michezo ya Ligi Kuu, ni lazima zitamke mashindano hayo kuwa ni “Ligi Kuu ya Vodacom”.

d-    Kwamba vituo vya televisheni vitakavyotaka kutangaza moja kwa michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom, ni lazima viingie mkataba na TFF ambao utaaridhiwa na klabu husika. Kwa sasa, kituo cha televisheni cha Star TV hakitaruhusiwa kurusha matangazo ya moja kwa moja ya michezo hiyo hadi hapo mkataba utakaposainiwa na tunatumaini mkataba huo utasainiwa kabla ya mechi za kesho na hivyo kuwapa fursa wapenzi wa soka wa maeneo mbalimbali kuendelea kushuhudia Ligi Kuu ya Vodacom.

e-    Kwamba vituo vya televisheni vitakavyotaka kuchukua picha kwa ajili ya habari zinaruhusiwa kufanya hivyo. Endapo kituo hicho kitaonyesha mchezo uliorekodiwa, hatua zitachukuliwa dhidi ya kituo hicho.

f-     Kamati inaomba radhi kwa usumbufu uliosababishwa na uamuzi huo, lakini inazidi kusisitiza kuwa uamuzi huo ulifanywa kwa lengo zuri la kuendelea kutafuta vyanzo vya fedha vitakavyoziwezesha klabu kujimudu kiuchumi na kuifanya Ligi Kuu ya Vodacom iendeshwe kwa ubora zaidi.

2.    Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Kim Poulsen amerejea Dar es salaam baada ya kufanya ziara kwenye visiwa vya Pemba na Unguja ambako alishuhudia mechi sita za Ligi Kuu ya Grand Malta kuanzia Oktoba 19, 2012 hadi Oktoba 26, 2012 visiwani Zanzibar. Poulsen alishuhudia mechi baina ya Falcom na Bandari iliyoisha kwa Falcom kushinda kwa mabao 3-1 na pia mechi baina ya Duma na Bandari ambayo iliisha kwa Bandari kuibuka na ushindi wa mabao 2-0. Mechi hizo mbili zilifanyika kisiwani Pemba.

Poulsen pia alishuhudia mechi zilizofanyika kwenye Uwanja wa Amaan kisiwani Unguja ambako Mtendeni iliibwaga Chipukizi kwa mabao 2-1; Mundu na Jamhuri (0-1), KMKM na Zimani Moto (1-0); na Mafunzo dhidi ya Chuoni iliyoisha kwa Mafunzo kulala kwa mabao 3-0.

Poulsen amefurahishwa na ziara hiyo na kusema kuwa ni kitu kizuri kwake na kwa soka la Tanzania kwa ujumla. Poulsen alisema kuwa amefurahishwa na mapokezi aliyopata visiwani Zanzibar na kukishukuru Chama cha Mpira wa Miguu cha Zanzibar (ZFA) kwa ushirikiano mkubwa alioupata wakati wote akiwa Zanzibar.

Hata hivyo, Poulsen alisema hawezi kueleza kwa sasa kama ameona wachezaji anaoweza kuwaita kwenye kikosi cha Taifa Stars, lakini akasema amevutiwa na viwango vya wachezaji wengi.

3.    TFF inapenda tena kuihimiza klabu ya Yanga kumalizana na mchezaji wake wa zamani, John Njoroge Mwangi kabla ya Novemba 2, 2012 ili ijiepushe na adhabu kaili inayoweza kuchukuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu (FIFA). Kwa mujibu wa barua ya FIFA, iwapo Yanga haitakuwa imemlipa mchezaji huyo na kusiwepo na mawasiliano yoyote, shauri hilo litawasilishwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya FIFA itakayokutana Novemba 14, 2012 kutathmini hukumu iliyotolewa mapema Januari mwaka huu.

4.    Mchezo namba 10 wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) baina ya Morani na Polisi Tabora uliokuwa uchezwe Kiteto mjini Tabora Oktoba 31, 2012, sasa utachezwa Novemba 01, 2012 baada ya treni ambayo Morani walikuwa wakisafiria kutoka kupata matatizo njiani wakati wakitoka Kigoma ambako walicheza na Kanembo.

5.    TFF inapenda kutoa ufafanuzi wa taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari leo, likiwemo gazeti la Habari Leo na Daily News, vikimnukuu rais wa TFF, Leodegar Tenga akisema kuwa amewataka watu wanaotaka kugombea uongozi wa shirikisho watangaze nia ili wapate kujadiliwa. Waandishi walioandika habari hiyo hawakumnukuu vizuri Rais Tenga wakati akizungumzia masuala ya uchaguzi na hivyo kupotosha maana nzima ambayo Ndg. Tenga alitaka iwafikie wapenzi wa michezo na hasa mpira wa miguu. Rais Tenga alivitaka vyombo vya habari vianzishe mjadala utakaowashirikisha wapenzi wa mpira wa miguu ili waelezee wanatarajia nini katika miaka ijayo na hivyo kuwafanya viongozi watakaochaguliwa kufanya kazi kwa utashi wa maoni hayo ya wananchi. Tunaelewa kuwa Rais Tenga ni muumini wa kuheshimu katiba, sheria na kanuni na hivyo hawezi kutoa kauli ambayo inakiuka mchakato wa uchaguzi wa TFF kwa kuwataka wanaowania uongozi kutangaza nia sasa badala ya kusubiri muda wa kikanuni ufike. Ikumbukwe katika kikao chake na wahariri aliwahi kuulizwa swali kama hilo na akasema kuwa akijibu lolote atakuwa amekiuka kanuni za uchaguzi kwa kuwa itamaanisha anaanza kampeniu kabla ya muda. Ni vizuri waliohusika wakafanya masahihisho ili kuzuia habari zao kutafsiriwa tofauti na wadau wa mpira wa miguu na hivyo kuweka uwezekano wa kuvuruga mchakato wa uchaguzi.

6.    TFF imebadilisha tarehe ya kuanza kuchukua fomu kwa watu wanaotaka kugombea uongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Dar es salaam (DRFA) kwa lengo la kuhakikisha kuwa mchakato wa uchaguzi unafanyika kwa mujibu wa kanuni. Kamati ya Uchaguzi ya DRFA ilitangaza jana kuwa uchukuaji fomu ungeanza leo, lakini DRFA iliandikiwa barua jana kuelezwa kuwa mchakato huo sasa utaanza kesho na uchaguzi utafanyika Desemba 12, 2012.


Mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa DRFA utakuwa kama ifuatavyo:
30/10/2012                                         Kamati ya Uchaguzi DRFA kutangaza uchaguzi na nafasi
Zinazogombewa kwa mujibu wa katiba ya DRFA
31/10/2012                                         Kuanza kuchukua fomu za kugombea uongozi
04/11/2012                                         Mwisho wa kurudisha fomu ifikapo saa 10:00 alasiri
05-09/11/2012                                   Kamati ya Uchaguzi DRFA kupitia fomu za waombaji uongozi na
kutangaza matokeo na kubandika kwenye mbao majina ya waombaji uongozi.
10-14/11/2012                                   Kutoa fursa ya pingamizi dhidi ya waombaji uongozi. Pingamizi
ziwasilishwe kwa katibu wa Kamati ya Uchaguzi DRFA na
wawekaji pingamizi wazingatie Ibara ya 11 (2) ya Kanuni za
Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
15-17/11/2012                                   Kujadili pingamizi, usaili na kutangaza matokeo ya usaili na
kuwajulisha kwa maandishi.
18-20/11/2012                                   Kukataa rufaa dhidi ya maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA

21-25/11/2012                                   Rufaa kusikilizwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na kutangaza
matokeo ya rufaa (Kama hakuna rufaa, Kamati ya Uchaguzi ya
DRFA kutangaza majina ya wagombea na nafasi wanazogombea
na kuanza kampeni).
26/11/2012                                         Baada ya maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Kamati ya
Uchaguzi ya DRFA kutangaza majina ya wagombea na nafasi zao
na kuanza kwa kampeni

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI WAGOMA

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Kimnyaki iliyopo wilayani Arumeru wakiwa mbele ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha wakidai kuondolewa kwa Mkuu wa shule yao kwa madai ya kuchelewesha wanafunzi wa kidato cha Nne kufanya mitihani.
Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Kimnyaki wakiwa wamekusanyika mbele ya ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha wakidai kuondolewa kwa Mkuu wao wa shule kwa madai ya kuwachelewesha wanafunzi wa kidato cha Nne kufanya mitihani

Monday, October 29, 2012

TRENI YA ABIRIA YAANZA KAZI JIJINI DAR NAULI NI SHILINGI 400 TU

Abiria treni ya kwanza kusafiri na wakiwa ndani ya treni ya abiria inayotoa huduma zake kutoka Ubungo Mziwa hadi Stesheni jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi.

USAFIRI WA TRENI KAMA DALADALA WAANZA JIJINI DAR ES SALAAM NAULI NI SHILINGI 400


Abiria wa mwanzo wa kutumia treni kwa usafiri wa ndani ya jiji ;a Dar es Salaamkwa kutumia reli ya Kati wakiteremka katika kituo cha Stesheni nauli kwa kila mtu ni shilingi 400/-
Treni ya kwanza kuteremsha abiria kwa kutumia usafiri wa kawaida kutoka Ubungo Maziwa hadi Stesheni jijini Dar es Salaam. Usafiri huu utakuwa ni mkombozi kwa wakazi wa Ubungo, Tabata na Buguruni,

Sunday, October 28, 2012

UMOJA WA VIJANA WA CCM WATWANGANA MANGUMI

Baadhi ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM wakiwa wamemshikilia mmoja wa vijana wanaompinga Mwenyekiti mpya wa Umoja huo, Khamis Sadifa Juma na viongozi wenzake,
Baadhi ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM wanaomuunga mkono Mwenyekiti wa Taifa wa umoja huo aliyechaguliwa hivi karibu mjini Dodoma wakimpga mangumi mmoja wa wanachama hao wanaopinga matokeo ya uchaguzi huo wa Mwenyekiti huyo kwa madai kuwa rushwa imetembea. Mpambano huo ulikuwa makao makuu ya umoja huo jijini Dar es Salaam
Wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM wakitwangana mangumi baada ya kundi moja linalopinga ushindi wa Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja huo kwenye mapokezi yaliyofanyika Makao Makuu ya Umoja huo jijini Dar es Salaam

PAMBANO LA MATUMLA NA MKENYA

Maofisa wa TPB wakiwa wanatafakari juu ya pambano la Matumla na Mkenya linalofanyika Mtwara

Bondia Rashid Matumla akipima uzito tayari kwa kupambana na Mkenya katika pambano lao lililotarajiwa kufanyika mjini Mtwara.

Friday, October 26, 2012

MELI YA KIVITA KUTOKA UINGEREZA YATIA NANGA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Askari wa Uingereza wakinyesha mfano wa namna ya kuwakabili maharamia wakati meli yao inayofanya doria Mashariki ya Kati ilipotia nanga katika bandari ya Dar es Salaam

Askari wa Uingeza waliopo kwenye meli ya kivita inayofanya patro kwenye bahari eneo la  Mashariki ya Kati wakizungumza na waandishi wa habari kwenye meli yao iliyotiananga katika bandari ya Dar es Salaam.

ASKARI WA UINGEREZA WA KIKOSI KINACHLINDA USAMA MASHARIKI YA KATI WAWASILI DARESSALAAM NA MELI YA KIVITA

Askari wa Kikosi cha kulinda usalama Mashariki ya Kati wakionyesha jinsi ya kuwakabili maharamia kwenye kwenye bahari.

A
Askari wa Uingereza kikosi kinachilinda usalama Mashariki ya Kati wakionyesha namna ya kumdhibiti haramia

Askari wa Jeshi la Maji la Uingereza wanaofanya doria katika ukanda wa Mashariki ya Kati wakionyesha jinsi ya kumdhibiti haramia wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Thursday, October 25, 2012

Mheshimiwa Hamad Rashid ateuliwa kuwa mjumbe kamati ya ukaguzi wa Hesabu za ndani IPU

Mheshimiwa Hamad  Rashid Mohamed akitoka katika mkutano na  Mwenyekiti wa kamati ya maswala ya Ulinzi na Usalama wa kimatifa Mhe. Saber Chowdury kutoka Bangladesh mara baada ya mjadala huo.
Mbunge wa Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Mkutano wa Chama cha Mabunge Duniani Mhe. Hamad Rashid Mohamed ameteuliwa na kamati tendaji ya chama cha Mabunge duniani (IPU) kuwa mjumbe wa kamati ndogo ya ukaguzi wa ndani kwa mahesabu ya mwaka 2013 ya chama hicho.
Uteuzi huo ulifuatia pendekezo la umoja wa Mabunge ya Afrika lililowasilishwa na katibu mkuu wake Koffi N’Zi tarehe 22 Oktoba, 2012 kufuatia kikao cha wajumbe wa umoja wa Mabunge ya Afrika kumchagua Mhe. Hamad kuwakilisha Afrika kuwania pendekezo hilo mbele ya kamati tendaji ya chama hicho.
Mhe. Hamad Rashid Mohamed, hii ni mara ya pili kuiwakilisha Tanzania na Afrika katika kamati mbalimbali za IPU ambapo mwaka jana katika Mkutano uliofanyika Mjini, Benn, Uswis, alichaguliwa kuwa mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi ya IPU cheo ambacho anakitumikia hadi hivi sasa.
Katika kamati hiyo ya ukaguzi wa ndani, Mhe. Hamad Rashid atafanya kazi pamoja na mjumbe mwingine aliyeteuliwa Mhe. Duarte Pacheko kutoka Ureno, ambapo wanatarajia  kutoa taarifa ya kazi yao mwaka 2014 katika mkutano mkuu wa IPU.
Katika hatua nyingine, Wabunge vijana wametakiwa kuwa chachu ya maendelo katika nchi zao kwa kushawishi kutengeneza mazingira ya upatikanaji wa ajira kwa vijana katika kipindi hiki cha uchumi wa kitandawazi.
Hayo yamesemwa jana na Mtaalamu wa maswala ya ajira kutoka shirika la la kazi la umoja wa mataifa (ILO) alipo toa maada katika mjadala wa Wabunge Vijana kujadili na namna ya kupunguza ajira kwa vijana hususani katika kipindi hiki cha uchumi wa utandawazi.
Mtaalamu huyo amesema ni wajibu wa wabunge kuwa na ushawishi mkubwa kwa serikali zao na baadhi ya taaisisi zinazotoa ajira ili kuwa na sera madhubuti kwa ajira za vijana hususani wanaomaliza vyuo kwa lengo la kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.
Amesema hivi saa duniani, zaidi ya asilimia 60 ya watu wote duniani ni vijana, na wengi wao wanakabiliwa na tatizo la ajira swala ambalo ni hatari kwa maendelo ya nchi nyingi duniani.
Wakichangia mada hiyo wabunge wengi walikubaliana dunia kuwa na tatizo la ajira na hususani kwa kushawishi serikali zao kuwa na sera madhubuti zenye kutatua tatizo la ajira kwa vijana katika nchi zao.
Mmoja wa wabunge kutola Denmark akichangia maada hiyo, amesema yeye anatoka katika mojawapo ya nchi zenye tozo kubwa la kodi katika sekata mbalimbali duniani, lakini wao kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa kupunguza tatizo la ajira kwa vijana kwa kuweka sera mathubudi zenye kuhakikisha kuwa vijana wanapata ajira mara tu wamalizapo shule.
Anasema moja wapo ya sera hizo ni pamoja na kuwa na kodi kubwa sana kwa mashirika au kampuni ambayo hayatoi idadi kubwa ya ajira kwa vijana au ambayo hayazingatii ajiri kwa  vijana. Pamoja na hilo, serikali ya Denmark imeweka utaratibu wa kutoa punguzo la kodi kwa mashirika au Makampuni yenye sera ya kuajiri vijana kutoka vyuoni ambapo hivi sasa ni asilimia 6% tu ya watu kutoka Denmak hawana ajira.
Tatizo hili limejitokeza sana katika chi za afrika, Asia na Latini Amerika ambapo Mbunge  kutoka Namibia akichangia mada hii amesema nchini kwake tatizo la ajira ni zaidi ya asilimia 52 na mashirika mengi na makampuni yanayojishughulisha na biashara kwa lengo la kupata faida, huona ni hatari sana kuajiri vijana wanaotoka kazini kwa kuwa wengi wao hawana uzoefu hivyo kufanya swala la uzalishaji kupungua kutokana na mda mwingi kutumika kufanya mafunzo kazini, jambo ambalo limepingwa vikali na wajumbe kutoka Afrika kusini, Tanzania, Norway na Maldives.

Mbunge David Kafulila aliyeshiriki semina hiyo kutoka Tanzania, amesema sio kweli kwamba serikali zetu zitafanya kila kitu kutoa ajira kwa vijana,  akichangia mada hiyo, kafulila alisema “ swala hapa ni kutengeneza mazingira ya kuwa na soko la ajira kwa vijana mara tu wamalizapo shule, sasa ni jukumu letu kushawishi serikali zetu kuwa na sera rafiki zenye kuweka mpango wa kutengeneza ajira kwa vijana” .
Kafulila aliongeza kuwa, mfano ni serikali zetu kuanzisha mikakati mipya ya maendeleo yenye kulenga kutoa elimu kulingana na soko la ajira, pamoja na kuvutia wawekezaji katika sekta muhimu zenye kutoa ajira kwa vijana.
Akitoa mfano wa Tanzania, Kafulila anasema hivi sasa sekta ya gesi, mafuta na Kilimo Tanzania ndiko soko kubwa la ajira liliko na lengo lao kama wabunge vijana Tanzania watahakikisha kuwa wanaishawishi sana serikali kuwa na sera ya jira kwa vijana kwa wawekezaji wote wanowekeza katika sekta hizi pamoja na kuongeza idadi ya vyuo vyenye kutoa elimu kulingana na mahitaji ya sekta hizi kuliko kuwa na wataalam wengi kutoka nje wanaokuja kufanya kazi Tanzania kwa kuwa kuna uchache wa wataalam katika sekta hizi.
Tatizo lililopo sasa ni kwamba nchi zetu ziache utaratibu wa kuongeza idadi ya vyuo vinavyotoa elimu inayofanana bila kuangalia mahitaji ya soko, kwani kuwa na idadi kubwa ya wasomi kwa fani moja tu nchini ni tatizo kubwa katika maendeleo ya nchi. 

Mkutano wa 127 wa IPU unaendelea leo hapa mjini Quebec ambapo mojawapo ya warsha itakayofanyika ni pamoja na ile inayosema “Kinga za Wabunge, ni Mzigo au ni kwa manufaa?
    

Wateja wa Airtel sasa kulipia Kodi kwa Airtel Money

Mkurugenzi wa Biashara za Mashirika wa Airtel bi Irene Madeje Mlola (Kulia) akifafanua jambo wakati wa uzinduzi wa Huduma itakayowawezesha wateja wa Airtel kulipa kodi ya mapato na Majengo kwa kupitia Huduma ya Airtel Money,pichani katikati ni Mwakilishi wa Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania bw Saleh Mshoro akiongea na kushoto ni  Kaimu Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi bwn Allan Kiula.


Wateja wa Airtel sasa kulipia Kodi kwa Airtel Money
·         Kulipia kodi ya mapato na majengo
·         Airtel na TRA kuwezesha ukusanyaji na ongezeko la mapato

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayotoa huduma za mawasiliano yenye gharama nafuu zaidi na mtandao wenye wigo mpana leo imezindua mwendelezo wa huduma za Airtel kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwawezesha wateja wake nchi nzima kulipia Kodi kupitia huduma ya Airtel Money. Hii imekuja wakati huduma za pesa kutumia simu zimekuwa zikibadilisha huduma za kibiashara na kuongeza ufanisi.
Kwa kupitia huduma ya Airtel money na ushirika na Mamlaka ya Mapato Tanzania Airtel wateja wa makampuni hayo wataweza kulipia kodi ya mapato na majengo kupitia Airtel Money.
Akiongea wakati wa uzinduzi uliofanyika makao makuu ya kampuni ya Airtel, Mkurugenzi wa Biashara za Mashirika bi Irene Madeje Mlola alisema” Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kuleta ufanisi na mapinduzi katika sekta ya mawasiliano nchini. Leo tuna furaha kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwezesha wateja wake kulipa kodi kwa kupitia huduma ya Airtel Money.  Airtel money ni huduma iliyotengezwa kukithi mahitaji ya wateja wetu na hii ni hatua nyingine muhimu kwa Airtel kutumia miundo mbinu tuliyonayo na TRA katika kuhakikisha wanaboresha huduma zao. Sasa walipaji wa kodi wadogo na wakubwa wanalipia kodi zao kwa urahisi wakiwa katika biashara zao na nyumbani”
“Mpaka sasa takribani nusu ya wateja wa Airtel wamejiunga na kutumia huduma ya Airtel money, huduma iliyo rahisi, iliyojitosheleza, salama na nyenye kutoa nafasi kufanya miamala mbalimbali ikiwemo malipo ya bidhaa mbalimbali. Kwa kupitia huduma ya Airtel money inayotoa huduma nyingi zaidi ya kutuma pesa tumeona maisha ya watanzania wengi yakibadilika kila siku na biashara zao kuwa na ufanisi zaidi aliongeza Madeje.”
Kwa upande wake Kamishina Msaidizi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania bw Rished Bade alisema” Tunayofuraha kuzindua huduma yenye kutumia mfumo wa teknolojia ya malipo ya uhakika na salama kwa wateja wetu nchi nzima.
Uzinduzi wa leo ni udihirisho wa juhudi za Mamlaka katika kuongeza uboreshaji katika huduma za malipo ya kodi na ukusanyaji wa mapato.Tunategemea kwa kupitia huduma ya Airtel Money kutawezesha ulipaji wa kodi kwa wakati na kuwahamasisha watanzania wengi zaidi kulipia kodi zao za mapato na majengo. TUnategemea kuona ongezeko kubwa la wafanya biashara wadogo na wakati ambao leo hii wanalipia malipo ya kodi kwa kupitia maofisi na vituo mbalimbali vya kodi nchi nzima.
Akiongelea kuhusu njia ya kulipia kodi hizo kwa njia ya simu Meneja Uendeshaji Airtel Money Asupya Naligingwa alieleza”Kulipia kodi ya majengo au mapato mteja wa Airtel atatakiwa kupiga namba  *150*60#  kisha
  1. Atachagua Lugha
  2. Atachagu malipo ya bili
  3. Lipa Bili
  4. Atachagu “JIna la fumbo” MAJENGO”
  5. Ingiza kiasi cha fedha unachotaka kulipia
  6. Ingiza neno la siri
  7. Ingiza namba ya akaunti ya Mamlaka ya Mapato (TRA) kisha bonyeza OK na utapokea meseji(SMS)itakayothibitisha malipo yako ”
Huduma ya Airtel Money service inayopatikana kwa kupiga  *150*60#  inawawezesha wateja kulipia huduma mbalimbali zikiwepo kama vile za kulipia bili za maji na umeme,bidhaa na huduma mbalimbali kama vile  bima,kununua muda wa maongezi,miamala ya huduma za kibenkiikiwemo kuweka na kupokea kutoa na vile vile kulipia huduma nyingine nyingi.
Airtel Money ni huduma inayopatikana masaa 24, siku 7 za wiki kutoka katika simu na ni salama ya uhakika na rahisi kutumia. Kinachohitajika ni kitambulisho na usajili wa simu yako ili kuweza kupata huduma hii katika maduka na mawakala wote waliopo nchi nzima.



Mwakilishi wa Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania  Saleh Mshoro na  Mkurugenzi wa Biashara za Mashirika wa Airtel, Irene Madeje Mlola na Kaimu Mkurugenzi wa huduma na Elimu kwa Mlipa kodi, Allan Kiula kwa pamoja wakionyesha kipeperushi  wakati wa uzinduzi wa Huduma itakayowawezesha wateja wa Airtel kulipa kodi ya mapato na Majengo kwa kupitia Huduma ya Airtel Money. Uzinduzi huu ulifanyika leo katika makao makuu ya Airtel Morocco.

KATIBU WA BAKWATA ARUSHA AJERUHIWA

Katibu wa Bakwata mkoa wa Arusha, Abdulkarimu Jonjo akiwa katika wodi ya majeruhi katika hospitali ya mkoa Mount Meru baada ya kujeruhiwa na bomu lililotupwa na watu wasiojulikana akiwa amelala nyumbani kwake majira ya saa 6.30 usiku

Wednesday, October 24, 2012

AIRTEL YAZINDUA PROMOSHENI YA JIPATIE MARA TANO”

Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania Sam Elangalloor akiongea  na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa promosheni ya “Jipatie Mara 5” inayowawezesha wateja wa Airtel kupata mara tano ya wastani wa kiwango cha pesa watakayotumia kila siku ikiwa ni sawa na 500% bonus ya muda wa maongezi. Uzinduzi huo umefanyika leo katika ofisi za makao makuu ya Airtel morocco

DR SHEIN AKIMPONGEZA MWENYEKITI MPYA WA UVCCM KHAMIS SADIFA JUMA

Dk. Sheni akimpongeza Khamis Sadifa Juma, baada ya kutangazwa Mshindi wa kuwa Mwenyekiti mpya wa UVCCM Taifa, katika uchaguzi uliofanyika  mjini Dodoma.

KHAMIS SADIFA JUMA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA WA UVCCMKhamis Sadifa Juma,

Khamis Sadifa Juma, baada ya kutangazwa Mshindi wa kuwa Mwenyekiti mpya wa UVCCM Taifa, katika uchaguzi uliofanyika jana mjini Dodoma.